Historia ya Kiswahili Nchini Rwanda: Kielelezo cha Nafasi ya Utashi wa Kisiasa katika Ustawi wa Lugha ya Kiswahili

Wallace Mlaga

Abstract


Makala hii inajikita kuonesha namna ambavyo utashi wa kisiasa umekuwa na umuhimu katika ustawi wa lugha ya Kiswahili nchini Rwanda. Ili kuonesha vema kuwapo kwa utashi wa kisiasa, hususan katika zama za sasa, makala inaitalii historia fupi ya Kiswahili nchini Rwanda, kuanzia kipindi cha ukoloni mpaka sasa. Makala inatambua zama za sasa kuwa zinaanzia mara baada ya mauaji ya kimbari (mwaka 1994) dhidi ya Watutsi hadi sasa. Ni katika kipindi hiki, ndipo mdhihiriko wa utashi wa kisiasa unabainishwa kwa mifano. Makala inabainisha pia kuwa ili kuwe na utashi wa kisiasa, lazima ziwepo sababu za msingi za kuleta utashi huo wa kisiasa. Pia inabainisha kuwa hata baada ya utashi wa kisiasa kuwapo, lazima kuwe na sababu zitakazohakikisha utashi huo wa kisiasa unaendelea kuwapo. Mwishoni kabisa makala inaonesha changamoto zinazokabili ustawi wa Kiswahili nchini Rwanda pamoja na mapendekezo ya nini kifanyike katika kutatua changamoto hizo.


Full Text:

PDF

Refbacks

  • There are currently no refbacks.