Dhima ya Lugha ya Mawasiliano katika Jamii: Kiswahili na Mkakati wa Usomaji kuelekea Umajumui wa Kiafrika

Aldin K Mutembei

Abstract


Dhima ya lugha ya mawasiliano imejadiliwa na wanazuoni kadhaa. Wengi wameiangalia kama yenye kuongelea masuala ya jamii inamochipuka wakiihusisha na fasihi, au ile yenye kutumia lugha za picha au kitaswira katika kuumba maana iliyokusudiwa. Makala hii inalenga mambo mawili ya msingi. Mosi, ni kuangalia dhima ya lugha ya mawasiliano katika baadhi ya kazi za kifasihi zinazovuka mipaka ya jamii zinamochipuka na pili, ni kuiangalia ikiwa lugha hii inao uwezo wa kutabiri yale yatakayokuja. Katika lengo la pili, makala inakwenda hatua moja zaidi na kuangalia ikiwa suala la Umajumui wa Kiafrika linaweza kujengwa na namna ya usomaji chanya wa kazi za kifasihi. Kwa hiyo, makala inajadili dhana ya “usomaji” kwa maana pana zaidi ya kuangalia maandishi na kupata maana. Katika mjadala wa vipengele hivyo, makala hii itatumia nadharia ya Thieta ya Walalahoi (Theatre of the Oppressed) kwa mujibu wa mawazo ya Boal (2008). Mawazo ya Boal, ndiyo yatakayotuongoza kufafanua maana ya “usomaji” kwa mujibu wa makala hii. Makala inaonesha kuwa Umajumui wa Kiafrika unaweza kujengwa na kuimarishwa kupitia katika usomaji wa kazi za kifasihi wenye kulenga ukombozi. Mawasiliano katika lugha ya Kiswahili na baadhi ya kazi za Kifasihi za Kiswahili yanatolewa kama mfano wenye kuweza kutumika katika kujenga Umajumui wa Kiafrika.


Full Text:

pdf

Refbacks