Changamoto za Istilahi katika Uandishi wa Tasinifu za Uzamili wa Kiswahili Tanzania

Arnold B.G Msigwa

Abstract


Uthabiti wa taasisi yoyote ya elimu ya juu hasa katika ngazi ya Chuo Kikuu unatokana na uimara wa programu zitolewazo katika taasisi husika na ubora wa wahitimu katika ngazi husika. Kuimarika kwa programu kama za Umahiri na Uzamivu ni sifa mojawapo ya taasisi ya elimu ya juu. Kuimarika huko hakutawezekana kama eneo la istilahi za kitaaluma zinazotumika kwa uwanja husika isimu/fasihi na methodolojia ya utafiti hazitakuwa sanifu na thabiti. Hivyo, makala haya yanafafanua changamoto za kistilahi katika pragramu za M.A. (Kiswahili) na PhD (Kiswahili) katika TATAKI kwa uzoefu wa miaka mitano. Swali linaloibuliwa na makala haya ni je, kutakuwa na usanifu wa program kama usanifishaji wa istilahi haujafanywa na taasisi husika. Mwito wa makala haya kwa watawala wa TATAKI na Chuo Kikuu kwa ujumla wake, ni kwamba, hima usanifishaji wa Istilahi katika Kiswahili hasa katika eneo la methodolojia ufanyike haraka kabla jahazi kuzama.

 


Full Text:

pdf

Refbacks

  • There are currently no refbacks.