Mulika Journal

MULIKA ni jarida la taaluma ya Lugha na Fasihi ya Kiswahili. Jukumu lake kuu ni kukusanya na kusambaza maarifa yanayohusu Lugha na Fasihi ya Kiswahili yaliyokitwa katika utafiti mpevu. Kutokana na mahitaji kwa baadhi ya watumiaji wa Kiswahili katika njanja nyingine, muda si mrefu jarida hili litaanza kupokea makala yaliyoandikwa kwa Kiswahili lakini yanahusu nyanja nyingine nje ya Lugha na Fasihi ya Kiswahili. MULIKA limeendelea kuwa daraja kati ya watumiaji wa Kiswahili popote walipo, na wataalamu wa Kiswahili katika shule za Sekondari na Vyuo vya Elimu ya Juu Afrika ya Mashariki na kwingineko. Jarida linapatikana katika tovuti ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kwa anwani ifuatayo: https://journals.udsm.ac.tz/index.php/mj