Dhima ya Ngoma katika Tamthiliya ya Kiswahili ya Kimajaribio: Mfano kutoka Lina Ubani (1984)

Aneth Kasebele

Abstract


Makala hii inachunguza dhima ya ngoma katika tamthiliya ya Kiswahili ya kimajaribio. Tafiti kuhusu matumizi ya ngoma katika tamthiliya ya Kiswahili ya kimajaribio zimeishia katika ngazi ya kubainisha tu pasi na kuchambua dhima zake. Kitendo cha kubainisha tu bila kuchambua dhima za ngoma katika tamthiliya ya Kiswahili ya kimajaribio hakioneshi umuhimu wa kipengele hicho cha kifasihi simulizi katika kazi za fasihi andishi. Data za makala hii zimepatikana maktabani kwa kusoma tamthiliya ya Lina Ubani kisha kuchambua dhima ya ngoma. Uchambuzi wa data za makala hii umeongozwa na Nadharia ya Uamilifu. Matokeo ya utafiti huu yameonesha kuwa ngoma ina dhima za kifani na kimaudhui katika tamthiliya ya Kiswahili ya kimajaribio.

http://doi.org/10.56279/jk.v86i1.4


Full Text:

 Subscribers Only

Refbacks

  • There are currently no refbacks.