Kukua kwa Matumizi ya Kiswahili Duniani na Utamaduni wake
Abstract
Makala hii iliwasilishwa tarehe 7 Julai 2023 mjini Copenhagen, Denmaki kuhusu maendeleo ya Kiswahili duniani. Makala inaeleza historia ya Kiswahili kwa muhtasari kwa kubainisha jamii za Waswahili, yaani wenyeji wa ukanda wa pwani wa Afrika Mashariki. Aidha, makala imetaja taasisi mbalimbali zilizoanzishwa kwa ajili ya kukuza Kiswahili. Kiswahili kinafundishwa katika taasisi mbalimbali katika maeneo mbalimbali duniani. Mwandishi amedokeza pia ukrioli wa utamaduni wa Kiswahili kwa kubainisha athari za mila mbalimbali katika Kiswahili, zikiwamo tasnia za sheria, kilimo, biashara na matibabu. Mwisho, mwandishi amedokeza msamiati wa Kiswahili kutoka katika lugha mbalimbali za Kiafrika na nje ya bara la Afrika, kutoka Ulaya na Asia.
Downloads
Published
2024-12-31