Mchango wa Kiswahili katika Kuleta Amani kwa Maendeleo Endelevu Barani Afrika

Authors

  • Tumaini Mahendeka Taasisi ya Elimu Tanzania

Abstract

Lengo la makala hii ni kueleza mchango wa lugha ya Kiswahili katika kuleta amani barani Afrika kwa ustawi wa maendeleo endelevu. Data zilikusanywa kwa njia ya mapitio ya nyaraka na zilichambuliwa kwa njia ya uchambuzi wa maudhui. Matokeo ya utafiti yanaonesha kwamba Kiswahili kina mchango katika kuleta amani barani Afrika kwa maendeleo endelevu kwani kinarahisisha mawasiliano na kuunganisha jamii za Kiafrika. Pia, Kiswahili kinawaunganisha watu wa makabila na itikadi tofauti na kuleta ushirikiano na maelewano miongoni mwao. Vilevile, Kiswahili kinatumika kama nyenzo ya kusuluhisha migogoro inayojitokeza katika jamii barani Afrika kutokana na ukabila kwani hakifungamani na kabila lolote. Hivyo, Kiswahili ni miongoni mwa tunu muhimu zinazotakiwa kuthaminiwa na jamii za Kiafrika kwa maendeleo endelevu.

 

http://doi.org/10.56279/jk.v87i2.6

Published

2024-12-31