Uchanganuzi wa Miundo ya Aristotle katika Tamthilia ya Kinjeketile

Authors

  • Richard Wafula Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Pamela Ngugi Chuo Kikuu cha Kenyatta
  • Sophie Okwena Chuo Kikuu cha Kenyatta

Abstract

Makala haya yanalenga kuweka wazi miundo ya Aristotle katika tamthilia ya Kinjeketile (1969). Kinjeketile ni tamthilia ya Kiswahili ambayo iliandikwa mwishoni mwa miaka ya 1960 wakati ambapo maigizo mengi yalichukua miundo ya Kimagharibi moja kwa moja. Huu ni wakati ambapo Waingereza walileta drama kwa madhumuni ya kujifurahisha wao wenyewe na kujikumbusha maisha ya kwao. Katika kufanya hivi, waliwatumia Watanzania hasa, watoto wa shule katika kuonesha tamthilia za akina Aristotle. Watanzania waliathiriwa kiasi cha kuweza kujishirikisha kikamilifu katika kutunga tamthilia na kuzionesha. Ebrahim Hussein aliandika Kinjeketile akitumia miundo ya kina Aristole, hasa tanzia ya Kigiriki ambayo hasa ndiyo msingi wa sheria za ki-Aristotle. Kutokana na masomo yake, Hussein aliweza kuiga miundo ya Aristotle katika utunzi wake

Downloads

Published

2021-08-17

Issue

Section

Articles