Majukumu na Athari za Nyimbo za Watoto katika enzi za Teknolojia ya Kidijiti: Mifano kutoka Nyimbo za Watoto nchini Tanzania

Steven Elisamia Mrikaria

Abstract


Karne ya 21 ina maendeleo makubwa katika nyanja ya sayansi na teknolojia ya habari na mawasiliano. Ni katika karne hii ambapo fasihi simulizi ya Kiswahili imeshuhudia kuingia kwa mambo mengi mapya yaliyougusa utanzu wake mkubwa na wa awali kabisa wa nyimbo za watoto za Kiswahili kiasi cha kuathiri uhalisia wake. Makala haya yanaangalia namna maendeleo ya teknolojia ya kidijiti yanavyoathiri nyimbo za watoto. Makala pia yanagusia kwa kifupi mustakabali wa nyimbo za watoto.

 


Full Text:

pdf

Refbacks

  • There are currently no refbacks.