Kiswahili Marekani

Lioba Moshi

Abstract


Nguvu ya Kiswahili inaonekana wazi kutokana na mafanikio yake na kutokana na kuwa chaguo la mamilioni ya wasemaji katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Kiswahili kimeenea sehemu mbalimbali za Afrika na Ulaya, kwa njia ya uhamiaji wa hiari na kwa sababu ya ukimbizi kutokana na vita mbalimbali vilivyoathiri wananchi hasa wale wa Maziwa Makuu na Somalia. Wakimbizi walijifunza Kiswahili kambini na wale ambao walizaliwa kambini, lugha yao ya kwanza imekuwa Kiswahili pamoja na lugha yao mama. Wafikapo ughaibuni, kwa kawaida, wanachagua Kiswahili kuwa lugha yao maalumu hapo wakijifunza lugha ya ugenini (yaani Kiingereza kwa Marekani, Uingereza na Kanada).


Full Text:

PDF

Refbacks

  • There are currently no refbacks.